Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), limeidhinishia Tanzania mkopo wenye masharti nafuu wa dola za Marekani milioni 567.25 sawa na shilingi za Tanzania Tril 1.3 kwa ajili ya kukabiliana na athari za ugonjwa wa UVIKO 19.
IMF iliidhinisha msaada huo wa dharura wa kifedha chini ya kituo cha mikopo ya haraka kwa lengo la kuunga mkono juhudi za mamlaka katika kukabiliana na janga hilo kwa kushughulikia gharama za haraka za kiafya, kibinadamu na za kiuchumi.
Mtazamo wa uchumi wa Tanzania umedorora kutokana na athari za janga la Uviko-19 pamoja na kuanguka kwa utalii baada ya vizuizi vya kusafiri, Ambapo uchumi unaripotiwa kupungua kwa ukuaji wa asilimia 4.8 mwaka 2020, na ukuaji unatarajiwa kubaki chini kwa mwaka 2021.
Tanzania inahitaji fedha za haraka karibu asilimia 1.5 ya Pato la Taifa kama mamlaka kutekeleza mpango mpana wa kupunguza athari za janga hilo na kuhifadhi utulivu wa uchumi mkuu mbele ya wimbi la Uviko-19.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa Serikali imeonyesha nia kwa kufuata sera za uchumi zinazofaa kushughulikia athari za janga hilo na kujitolea kuimarisha uratibu na uwazi ili kuhakikisha kuwa rasilimali hizo zinatumika katika kupambana na janga hilo.