Star Tv

Msichana mmoja aliyejulikana kwa jina la Neha Paswan, mwenye umri wa miaka 17, anadaiwa kupigwa hadi kufa na watu wa familia yake katika jimbo la kaskazini la Uttar Pradesh kwasababu hawakupenda vile anavyovaa jeans.

Mama yake, Shakuntala Devi Paswan, aliiambia BBC Hindi kwamba msichana wake alikuwa amepigwa vibaya na fimbo na babu yake na wajomba zake baada ya kutokea kwa mabishano nyumbani juu ya nguo zake anazovaa katika kijiji cha Savreji Kharg wilayani Deoria, moja ya maeneo yenye maendeleo duni katika jimbo hilo.

"Alikuwa amefunga siku nzima kwendana na dini. Wakati wa jioni, akavaa suruali ya jeans na juu akawa na top au aina ya fulana kufanya ibada zake. Wakati babu na bibi yake walipinga mavazi yake, Neha alijibu kwamba jeans zilitengenezwa kwa ajili ya watu kuvaa"- Mama yake alisema.

Shakuntala Devi alisema wakati binti yake akiwa amelala baada ya kupoteza fahamu, wakwe zake waliita gari wakisema wanampeleka hospitalini.

"Hawakuniruhusu niandamane nao kwa hivyo niliwatahadharisha jamaa zangu ambao walikwenda hospitali ya wilaya wakimtafuta lakini hawakumpata"-Aliongeza Mama yake Neha.

Asubuhi iliyofuata, Shakuntala Devi alisema, walisikia kwamba mwili wa msichana mmoja umepatikana ukininginia kutoka kwenye daraja juu ya mto wa Gandak unaopita eneo hilo.

Walipokwenda kuchunguza, waligundua mwili huo ni wa binti Neha.

Polisi wamewasilisha kesi ya mauaji na uharibifu wa ushahidi dhidi ya watu 10, akiwemo babu na nyanya wa Neha, ami, shangazi, binamu na dereva wa magari, Ambapo washtakiwa bado hawajatoa tamko lolote kwa umma.

Afisa mwandamizi wa polisi Shriyash Tripathi aliambia BBC Hindi kwamba watu wanne, pamoja na babu na nyanya, mjomba na dereva wa magari, wamekamatwa na walikuwa wanahojiwa.

 

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.