Star Tv

Mwanamfalme wa Saudia Muhammad Bin Salman ameidhinisha kutolewa kwa pesa milioni 3.74 za riyali, sawa na dola milioni 1 za kimarekani, ili zigawiwe kwa vijana 200 kama ruzuku ya kuoa.

Gazeti la serikali la Saudi Arabia limeripoti kwamba tangazo hilo lilitolewa na Shirika la habari la Saudia siku ya Jumapili.

Taarifa hiyo ilisema kuwa fedha hizo zitagawanywa kwa vijana wa kiume na wa kike kote nchini humo.

Limesema agizo la Mwanamfalme huyo ni katika juhudi za kuwasaidia yatima wenye ulemavu na watu wenye ulemavu ambao wamekuwa na shida ya kuoa.

Katika awamu ya kwanza ya mpango huo, riyali milioni 250 za msaafda zilisambazwa, kwa watu zaidi ya 26,000 kutoka maeneo tofauti ya nchi hiyo.

Licha ya kupewa pesa vijana watafundishwa jinsi ya kutumia pesa.

Mpango wa Mwanamfalme Muhammed Bin Salman ulianzishwa kwa lengo la kuimarisha uchumi na jamii ya watu wa nchi hiyo kuboresha maisha ya watu.
#ChanzoBBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.