Star Tv

Wazazi wawili wa watoto wa shule waliotekwa nyara katika eneo la Tegina katika jimbo la kati la Nigeria la Niger wamekufa kutokana na mshtuko, vimesema vyombo vya habari.

Wazazi hao walipatwa na mshtuko baada ya kupata taarifa ya genge la watu kuwateka wanafunzi kutoka kwenye shule yao Jumapili.

Wazazi hao walisemekana waliugua ghafla na kupoteza fahamu.

Watekaji nyara wanasemekana kuwa wamekuwa wakiwaomba kikombozi kabla ya kuwachilia watoto wao na wametishia maisha yao iwapo hawatalipwa, kulingana na taarifa.

Awali, Mkuu wa shule ya kiislamu aliiambia BBC kwamba alizungumza na watekaji nyara na wakamuhakikishia kuwa watoto walikuwa wazima na wenye afya.

Abubakar Alhassan alisema kuwa wanafunzi 136 hawajulikani walipo, wakiwemo watoto wake watano, baada ya kuhesabu idadi ya watoto kufuatia utekaji huo.

Aidha, Walimu watatu pia hawajulikani walipo. Hata hivyo, bado hakuna taarifa rasmi ya idadi kamili ya wanafunzi waliotekwa nyara. 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.