Rais Samia Suluhu Hassani amewaapisha mawaziri na manaibu waziri aliowateua.
Rais Samia amewaapisha Mawaziri hao pamoja na Manaibu Waziri katika ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.
Akiongea katika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma, wakati wa kuwaapisha Mawaziri walioteuliwa Rais Samia amesema kuwa sio jambo la busara wanaisasa kuanzisha kampeni za mapema.
"Nafahamu 2025 iko karibu na kawaida yetu Watanzania ama kote ulimwenguni inapoingia kipindi cha pili cha rais aliyepo watu kidogo mnakuwa na lile na hili kuelekea mbele..nataka kuwaambia acheni"-Alisema Rais Samia.
Aidha Rais Samia amewataka Mawaziri hao kufanya kazi kwa ushirikiano hasa katika masuala yanayohusu muungano kwani serikali ni moja.
Mawaziri hawalioapishwa leo ni kutokana na mabadiliko ambayo yamefanywa na Rais Samia Machi 31.