Wabunge, Mawaziri pamoja na Naibu Mawaziri walioteuliwa na Rais Samia Suluhu hapo Hassan jana Machi 31, wamekula viapo vyao vya uaminifu leo April 01,2021 bungeni Dodoma.
Miongoni mwao ni Liberata Mulamula ambaye ameteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika mashariki, Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mbarouk Nassor.
Aidha, Dkt. Bashiru Ally ambaye alikuwa Katibu Mkuu Kiongozi pamoja nayeamekula kiabo kama mbunge aliyeteuliwa na Rais.
Hapo jana Rais wa Tanzania Samia suluhu Hassan alifanya mabadiliko madogo katika baraza jipya la mawaziri wakati wa hafla ya kuapishwa kwa Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango, Ambapo Balozi wa Tanzania nchini Japan Hussein Yahya Katanga aliteuliwa kushika nafasi ya Katibu Mkuu Kiongozi.