Mahakama ya Kimataifa ya Kesi za Jinai (ICC) leo Machi 30,2021 inatarajiwa kuamua rufaa iliyowasilishwa mbele yake na kiongozi wa waasi wa Jamhuri ya Kidemorasia ya Congo, Bosco Ntaganda, kupinga hukumu ya uhalifu wa kivita dhidi yake.
Kamanda huyo wa zamani, aliyepewa jina la utani la 'The Terminator', alihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela mwaka 2019 baada ya kupatikana na hatia ya makosa 18 ikiwemo mauaji, ubakaji na kutumia watoto kamawanajeshi.
Alikuwa mtu wa kwanza kushtakiwa na mahakama hiyo kwa tuhuma ya utumwa wa kingono.
Mashtaka hayo yalihusisha uhalifu uliotekelezwa katika eneo la Ituri lenye utajiri wa madini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo mwaka 2002 na 2003.
Aidha, Waendesha mashtaka wanaomba majaji kutoa adhabu kali zaidi.