Star Tv

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza siku 14 za maombolezo pamoja na bendera kupepea nusu mlingoti kufuatia kifo cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awamu ya tano Dkt. John Pombe Maguful kilichotokea Machi 17,2021.

Makamu wa Rais ametangaza msiba huo kupitia Televisheni ya Taifa (TBC) ambapo amesema kuwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli amefariki Dunia kutokana na maradhi ya moyo.

"Rais alilazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Machi 06, akaruhusiwa Machi 07. Kabla ya kupelekwa Hospitali ya Mzena Machi 14,2021".-Alisema Makamu wa Rais.

Kufuatia msiba huu wa taifa, Makamu wa Rais ametangaza siku 14 za maombolezo ambapo pia amesema bendera zitapepea nusu mlingoti.

Marehemu Rais Magufuli alizaliwa Oktoba 29,1959,  Alichaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 2015 na amefarika Machi 17, 2021 katika hatamu ya awamu ya pili ya urais wake.
#RIPRaisJohnPombeMagufuli

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.