Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi amewafuta kazi Wakuu wa majeshi, Ambao ni Jeshi la ardhini na angani.
Rais Nyusi amefikia hatua hiyo wakati nchi hiyo inapokabiliana na wanamgambo wa Islamic States Kaskazini na waasi wa wanamgambo wanaohusishwa na chama kikuu cha upinzani.
Katika taarifa iliyotolewa usiku Alhamisi rais hakutoa sababu ya kumfuta kazi Ezequiel Isac Muianga, Mkuu wa jeshi la ardhini, na Messias André Niposso, mkuu wa jeshi la anga.
Rais pia amemfuta kazi Kamanda na Naibu Kamanda wa chuo cha Mafunzo ya Kijeshi cha Marechal Samora Macheya.
Aidha Naibu Kamanda wa Taasisi ya mafunzo ya juu ya masuala ya ulinzi nchini humo pia amefutwa kazi.