Star Tv

Kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Papa Francis anayeendelea na ziara yake ya kihistoria nchini Iraq ametoa wito kwa viongozi na watu wa nchi hiyo kuepuka vurugu na mivutano ya kidini.

Papa Francis anafanya ziara ya siku nne nchini Iraq ambayo ni ya kwanza kufanywa na kiongozi wa Kanisa Katoliki kwenye taifa hilo la Mashariki ya Kati.

Usalama umeimarishwa kwa ajili ya kumlinda kiongozi huyo wa kanisa katoliki baada yakutokea mashambulio ya roketi na yale ya kujitoa muhanga katika siku za hivi karibuni nchini humo.

Wakati huo huo hatua za kiafya zinazingatiwa zaidi kutokana na hali ya maambukizi ya virusi vya corona yanayoongezeka nchini Iraq.

Baba mtakatifu atakutana na kiongozi wa madhehebu ya Shia nchini Iraq, Ayatollah Ali Sistani pamoja na pia atazuru miji minne ukiwemo mji wa Mosul ambako makanisa na turathi nyingine zimeharibiwa na wanamgambo wa itikadi kali.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.