Mwili wa balozi wa Italia aliyeuawa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika jaribio la utekaji nyara uliotibuka siku ya Jumatatu, umesafirishwa kwenda mjini Roma.
Luca Attanasio, mlizi wake Vittorio Lacovacci, na dereva wake raia wa DR Congo Moustapha Milambo, waliuawa katika shambulio lililofanywa dhidi ya msafara wa magari ya chakula ya Umoja wa Mataifa, Mashariki mwa nchi hiyo.
Ndege ya kijeshi ya Italia iliyokuwa imebeba majeneza mawili yaliyokuwa yamefunikwa bendera ya kitaifa ilitua katika uwanja wa ndege wa Ciampino mjini Roma na kupokelewa na Waziri Mkuu, Mario Draghi.
Mamlaka nchini DR Congo zimelaumu kundi la waasi wa Rwanda la FDLR kwa mauaji, Lakini pia kundi hilo limekanusha kuhusika na shambulio hilo.