Star Tv

Mwanasiasa wa upinzani na raia wa Rwanda anayeishi mafichoni nchini Afrika Kusini ameuawa kwa kupigwa risasi.

Ripoti zinasema Seif Bamporiki aliuawa alipokuwa akiwasilisha samani kwa mteja Jumapili mchana mjini Cape Town.

Haijabainika kama kifo chake kilichochewa kisiasa.

Aidha, Waliomvamia walichukua simu zake za rununu na waleti kabla ya kutoroka eneo la tukio, na hakuna aliyekamatwa kuhusiana na kisa hicho.

Bw. Bamporiki alikuwa mshirikishi wa chama cha Rwanda National Congress.

Msemaji wa chama hicho, Etienne Mutabazi ameiambia BBC kwamba mteja alikuwa amewasiliana na Bw. Bamporiki ambaye anaendesha duka la kuuza vitanda,  kuuliza kama ana kitanda cha kuuza.

"Mteja kisha aliomba kitanda hicho kupelekwa katika mji wa Nyanga na kuamua kutumia gari na Bwana Bamporiki na mwenzake kwenda eneo ambalo kitanda kilitakiwa kupelekwa"-Mutabazi.

Maelezo ya kile kilichotokea baada ya hapo bado hayajathibitishwa, lakini Bw. Bamporiki aliuawa kwa risasi moja ambayo ilipigwa kupitia dirisha la gari.

Mji wa Nyanga unafahamika kuwa moja ya miji hatari nchini Afrika Kusini, Ambapo wakati mmoja mji huo ulikuwa na idadi ya juu zaidi ya mauji kwa mwaka.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.