Star Tv

Kiongozi wa upinzani Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine, amemtaka jaji Mkuu kujiondoa katika kusikiliza shauri la kupinga kuchaguliwa tena Rais Yoweri Museveni.

Bobi Wine amemshutumu jaji Alfonse Owiny - Dollo kwa upendeleo kwa sababu ya ushirika wake na rais wa Uganda, Yoweri Museveni.

Mwanasiasa huyo wa upinzani pia anataka majaji wengine wawili wa mahakama ya juu kujiondoa kusikiliza shauri hilo kwa misingi hiyohiyo.

Majaji watatu hawajajibu chochote kuhusu shutuma dhidi yao.

Jaji Mkuu Owiny-Dollo alikuwa mwanasheria wa Rais Museveni mwaka 2006, kwa mujibu wa tovuti ya Nile Post.

Jaji Mike Chibita alikuwa msaidizi wa Museveni katika masuala ya sheria, wakati Jaji Ezekiel Muhanguzi ni ndugu wa Waziri wa Ulinzi Elly Tumwine kwa mujibu wa vyombo vya habari vya nchini humo.

Bobi Wine amedai kuwa watatu hao hawataweza kutenda haki iwapo watasikiliza shauri hilo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.