Polisi Mjini New York wameeleza kuwa Baba wa mwanamuziki wa miondoko ya kufokafoka, Nicki Minaj, 64, ameaga dunia baada ya kugongwa na gari kisha dereva kukimbia mjini New York.
Robert Miraj alikuwa akitembea kandokando ya barabara katika kisiwa cha Long siku ya Ijumaa na kugongwa na gari, kisha dereva wa gari hiyo aliendelea na safari, polisi katika kaunti ya Nassau imesema.
Miraj alipelekwa hospitalini ambako alithibitishwa kufariki siku ya Jumamosi.
Polisi wametaka shuhuda yeyote wa tukio hilo baya kujitokeza. Gazeti la the Guardian limeripoti .
Minaj, 38, kwa jina la Onika Tanya Miraj alizaliwa huko Trinidad na alikulia jijini New York City borough of Queens.
Aidha, Mwanamuziki huyo hajajitokeza kuzungumza chochote kuhusu kifo cha baba yake.