Star Tv

Polisi Mjini New York wameeleza kuwa Baba wa mwanamuziki wa miondoko ya kufokafoka, Nicki Minaj, 64, ameaga dunia baada ya kugongwa na gari kisha dereva kukimbia mjini New York.

Robert Miraj alikuwa akitembea kandokando ya barabara katika kisiwa cha Long siku ya Ijumaa na kugongwa na gari, kisha dereva wa gari hiyo aliendelea na safari, polisi katika kaunti ya Nassau imesema.

Miraj alipelekwa hospitalini ambako alithibitishwa kufariki siku ya Jumamosi.

Polisi wametaka shuhuda yeyote wa tukio hilo baya kujitokeza. Gazeti la the Guardian limeripoti .

Minaj, 38, kwa jina la Onika Tanya Miraj alizaliwa huko Trinidad na alikulia jijini New York City borough of Queens.

Aidha, Mwanamuziki huyo hajajitokeza kuzungumza chochote kuhusu kifo cha baba yake.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.