Star Tv

Rais wa Marekani Joe Biden amesema hatua ya Baraza la Seneti ya kumuondolea mashtaka rais wa zamani Donald Trump ya kuchochea vurugu kwenye majengo ya bunge ni jambo linalokumbusha kuwa demokrasia imedhoofika.

Biden ameyasema hayo saa chache baada ya Baraza la Seneti kushindwa kupata theluthi mbili ya kura ili kumtia hatiani Trump, anayekuwa kiongozi wa kwanza wa Marekani kushtakiwa mara mbili mbele ya Bunge.

Bwana Biden amesema mwenendo huo unaonesha jinsi demokrasia inavyochechemea na kuwatolea wito raia wa nchi hiyo kusimama kidete kulinda ukweli na kupinga aina zote za hadaa.

Katika kura ya jana maseneta 57 ikiwemo 7 kutoka chama cha Trump cha Republican, walipiga kura ya kumtia hatiani rais huyo wa zamani huku 43 wakikataa mashtaka dhidi yake.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.