Star Tv

Rais wa Uganda Yoweri Museveni, leo anaanza safari ya kutoka kijijini kwao akielekea mji wa Kampala ambapo atakuwa anasimama katika vituo kadhaa kwenye miji mbalimbali kutoa shukrani kwa wananchi.

Rais Museveni aliyeshinda tena uchaguzi wa urais wiki iliyopita ili kuongoza kwa muhula wa sita atasimama katika vituo saba akiwa njiani kurejea Kampala.

Msemaji wa serikali Ofwono Opondo ameandika taarifa za kina juu ya safari hiyo kwenye mtandao wa Twitter.

Safari hiyo ya Rais inawadia wakati wito umetolewa kwa serikali kuondoa kifungo cha nyumbani dhidi ya kiongozi wa upinzani Robert Kyagulanyi, maarufu kama Bobi Wine, ambaye anapinga matokeo ya uchaguzi.

Marekani imetoa wito wa kufanyika kwa uchunguzi katika madai ya wizi wa uchaguzi yaliyoibuliwa na upande wa upinzani ambao bado haujafanikiwa kuwasilisha ombi rasmi la kupinga matokeo.

Ofisi za upinzani zilivamiwa na jeshi na maafisa wa chama hicho wanasema nyenzo walizokuwa wanazikusanya kwa ajili ya kupinga matokeo ya uchaguzi walinyang’anywa na maafisa hao.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.