Star Tv

Rwanda imetoa agizo la kufunga tena shule zote za umma kuanzia Januari 18, 2021 leo Jumatatu.

Wizara ya Elimu imesema kuwa shule zote za chekechea, msingi na za sekondari za umma na za kibinafsi zitafungwa katika mji wa Kigali kama njia moja ya kukabiliana na usambaaji wa virusi va corona hasa mjini Kigali.

Pia, wanafunzi wa shule za bweni watasalia katika shule zao na wataendelea kupokea huduma muhimu.

Wizara hiyo pia imeongeza kuwa shule zote nje ya mji wa Kigali zitaendelea kufunza na shughuli zingine za masomo kwa kuzingatia hatua kukabiliana na ugonjwa wa Covid-19 na pia muongozo huo utapitiwa tena katika kipindi cha wiki mbili zijazo kulingana na tathmini ya huduma ya afya.

Watu 22 walikufa kutokana na Covid19 kwa muda wa siku 7 zilizopita na kuifanya idadi ya waliokufa kutokana na corona hadi kuifikia sasa kuwa 142.

Haya yanajiri wakati bado ikitekelezwa marufuku ya siku 15 ya usafiri wa umma kati ya wilaya na mji mkuu Kigali ambapo pia biashara zote nchini humo husitishwa saa kumi na mbili jioni.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.