Star Tv


Saudi Arabia imesema itafungua tena ubalozi wake nchini Qatar katika siku zijazo, kufuatia mkutano wa kilele wa wiki iliyopita ulioungwa mkono na Marekani, ambapo mataifa ya Ghuba yalikubaliana kumaliza mzozo wa miaka mitatu.

Mzozo huo ulianza mnamo mwaka 2017, pale Saudi Arabia, Umoja wa Falme za Kiarabu, Bahrain na Misri zilipoiwekea Qatar vikwazo vya kidiplomasia, kibiashara na vya kusafiri kwa madai kwamba inafadhili makundi ya kigaidi.

Mataifa hayo ya Kiarabu yameahidiana kuimarisha ushirikiano wao, ili kuongeza nguvu ya kupambana na Iran katika eneo la Mashariki ya Kati.

Hayo yakijiri, Marekani kwa mara ya kwanza imezitaja Bahrain na Umoja wa Falme za Kiarabu kama washirika wake wakuu wa usalama, kauli iliyowashangaza wengi.

Halikadhalika, Rais Donald Trump ametunukiwa tuzo ya hadhi ya juu na Mfalme wa Morocco kwa juhudi zake za kurejesha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Morocco na Israel.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.