Star Tv

Raia wa Uganda hii leo Januari 14,2021 wanapiga kura kumchagua rais na wawakilishi wapya wa bunge.

Akizungumza siku ya Jumatano mwenyekiti wa tume ya uchaguzi nchini humo jaji Simon Byabakama aliserma kwamba wapiga kura wa kiume ni zaidi ya milioni tisa huku wenzao wa jinsia ya kike wakiwa zaidi ya milioni tisa.

Katika uchaguzi huo rais Yoweri Museveni ambaye anatetea wadhfa wake anakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa mwanamuziki wa zamani maarufu Bobi Wine.

Bobi Wine ni mgombea ambaye amevutia idadi kubwa ya vijana nchini humo.

Rais Museveni anagombea muhula wa sita baada ya kuwa madarakani kwa miaka 35.

Hata hivyo rais Museveni anajivunia utawala wake wa muda mrefu ambapo amefanya baadhi ya maenedeleo.

Robert Kyagulanyi, maarufu Bobi Wine, anasema kuwa anawakilisha kizazi kipya cha vijana wa nchini humo, huku Yoweri Museveni mwenye umri wa miaka 76, akisema kuwa anasimamia ustawi.

Chanzo na BBC Swahili.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.