Star Tv

Uchunguzi umeanzishwa nchini Ufaransa baada ya kutoweka kwa mwanafunzi Msenegali mwenye kipaji ambaye alikuwa akisoma katika shule ya kifahari mjini Paris.

Mwanafunzi huyo Diary Sow hakurejea shuleni baada ya mapumziko ya Krismasi na kusababisha hofu Senegal na Ufaransa.

Akielezewa kama "mwanafunzi bora wa Senegal", Bi Sow alishinda tuzo kadhaa za kielimu na kuchapisha kitabu chake cha kwanza cha tamthilia mwaka jana.

Mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 20, hajaonekana tangu tarehe 4 Januari.

Raia wa Senegal wanaoishi katika mataifa ya kigeni wamekuwa wakimtafuta kupitia mitandao ya kijamii.

Huku watu mashuhuri wa Ufaransa ikiwa ni pamoja na mcheza filamu Omar Sy, wameshirikisha umma ombi lao la kutafutwa kwa Bi Sow kupitia mitandao ya Instagram na Twitter.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.