Star Tv

Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa amezungumzia vurugu zilizotokea Marekani baada ya wafuasi wa Rais Donald Trump kuvamia jengo la bunge Capitol Hill.

Rais Mnangagwa aliandika ujumbe kwenye mtandao wa Twitter kuwa Marekani haina "haki ya kimaadili kuadhibu nchi zingine kwa misingi ya demokrasia".

Alisema kuwa Marekani imeiwekea Zimbabwe "vikwazo vikali" vya kiuchumi.

Mnangagwa amempongeza rais mteule "Ningependa tena kumpongeza Rais mteule Joe Biden, kwa kuthibitishwa kuwa Rais wa 46 wa Marekani, Zimbabwe iko na imekuwa tayari ushirikiano wake kama marafiki na washirika wa Marekani kwa manufaa ya nchi zote mbili," Bwana Mnangagwa amesema.

Marekani na Umoja wa Ulaya zote zimeendeleza vikwazo vyao dhidi ya Zimbambwe kwa madai ya ukosefu wa demokrasia endelevu na mabadiliko ya haki za binadamu pamoja na kubanwa kwa vyombo vya habari.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.