Star Tv

Idadi ya wajumbe wa Republican imeongezeka, wakiungana na juhudi za Rais Donald Trump kupinga matokeo ya uchaguzi wa Marekani uliofanyika mwishoni mwa mwaka 2020.

Maseneta hao wamesema wanayakataa matokeo ya uchaguzi huo wakati Bunge litakapoandaa kikao wiki ijayo cha kuhesabu kura za wajumbe maalum maarufu kama Electoral College na kuidhinisha ushindi wa Rais mteule Joe Biden.

Seneta Ted Cruz wa jimbo la Texas ametangaza muungano wa maseneta 11 na maseneta wateule ambao wamedhamiria kuyapinga matokeo hayo katika kikao cha pamoja cha mabaraza yote mawili ya bunge Jumatano ijayo.

Kiongozi wa Warepublican katika Seneti Mitch McConell alikiomba chama chake kutojaribu kukibatilisha kile ambacho maafisa wasioegemea chama chochote wamesema ni uchaguzi uliokuwa wa huru na haki.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.