Star Tv

Israel itafanya uchaguzi wake wa nne katika kipindi cha miaka miwili baada ya vyama vikuu viwili katika serikali ya umoja kushindwa kuheshimu muda wa mwisho wa kutatua mzozo juu ya bajeti ya taifa.

Israel imeitisha uchaguzi huo mwezi Machi baada ya bunge kushindwa hapo jana kuidhinisha bajeti ya serikali ikiwa ndiyo muda wa mwisho uliopangwa kufanya hivyo.

Kampeni za uchaguzi wa nne wa bunge ndani ya miaka miwili, zitafanyika wakati Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu akiwa anakabiliwa na changamoto kadhaa.

Miongoni mwao ni hasira ya umma inayotokana na jinsi alivyoshindwa kukabiliana na janga la virusi vya corona, huku akiwa katikati ya kesi ya ufisadi, ya kwanza dhidi ya waziri mkuu wa Israel.

Mpinzani mkuu wa Netanyahu katika uchaguzi ujao ni Gideon Saar, mwanasiasa aliyejitenga kutoka katika chama chake cha Likud.

Utafiti wa maoni ya raia kabla ya uchaguzi unaonyesha kuwa Saar anamkaribia sana Netanyahu kwa umaarufu miongoni mwa wapiga kura.

Saa kadhaa kabla ya muda wa mwisho kumalizika, Netanyahu ambaye ni kiongozi wa vuguvugu la mrengo wa kulia la chama cha Likud, na mpinzani wake wa kisiasa Benny Gantz kutoka vuguvugu la mrengo wa kati la Blue na nyeupe, walilaumiana kila upande ukiutuhumu mwingine kusababisha mzozo huo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.