Star Tv


Marekani imeidhinisha chanjo aina ya Moderna kama chanjo ya pili ya corona nchini humo, baada idhini ya kusambazwa kwa dozi za chanjo hiyo kutolewa.

Mamlaka ya kusimamia usalama wa chakula na dawa (FDA) iliidhinisha chanjo hiyo iliyongenezwa Marekani karibu wiki moja iliyopita baada ya kuidhinisha chanjo ya Pfizer/BioNTech ambayo kwasasa inatolewa.

Marekani ilikubali kununua dozi milioni 200 ya Moderna, na milioni sita kati ya hizo huenda ziko tayari kusafirishwa.

Kamishna wa FDA Stephen Hahn amesema kuidhinishwa kwa dharura kwa chanjo hiyo siku ya Ijumaa kunaashiria ''hatua nyingine muhimu katika juhudi za kukabiliana na janga la kimataifa ".

Hatua ya kuidhinishwa kwa chanjo hiyo ilifikiwa baada ya jopo la wataalamu kupiga kura siku ya Alhamisi 20-0 huku wito ukitolewa kwamba ubora wa chanjo ya Moderna unazidi madhara yake kwa watu waliyo na umri 18 na zaidi.

Wadhibiti waliripoti mapema wiki hii kwamba chanjo ya Moderna ilikuwa salama na inafanya kazi kwa asilimia 94.

Rais wa Marekani Donald Trump,aliandika katika mtandao wake wa Twitter saa kadhaa kabla ya tangazo rasmi kutolewa alisema chanjo hiyo "imeidhinishwa kwa kishindo" na itaanza kusambazwa "mara moja”.

Huku Rais mteule Joe Biden, ambaye anajiandaa kupewa chanjo siku ya Jumatatu, amesema kuidhinishwa kwa chanjo za sindano za Pfizer na Moderna "kunatuhakikishia siku njema huko mbele".

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.