Star Tv

Wanamgambo wa kundi la Kiislamu la Boko Haram wametoa video mpya ambayo inasema wapiganaji wake wa Boko Haram ndio waliotekeleza mauaji ya wakulima 78 katika eneo la Zabarmari karibu na Maiduguri kaskazini mashariki mwa Nigeria.

Jumamosi, wanaume waliokuwa na silaha waliotumia pikipiki na kutekeleza shambulizi la kinyama dhidi ya wakulima wa mashamba ya mpunga.

Wakati huohuo, wabunge wa Nigeria wamefanya mazungumzo na rais Muhammadu Buhari juu ya mauaji hayo na Wabunge hao wamesema suala hilo ni la kupewa umuhimu mkubwa.

Katika video iliyoonekana na BBC, Abubakar Shekau, kiongozi wa kundi la Boko Haram–aliyefunika uso wake, alisema kundi hilo lilitekeleza shambulizi dhidi ya wakulima wa mashamba ya mpunga wikendi iliyopita.

Hilo linawadia wakati raia wa Nigeria wanaendelea kughadhabishwa na mauaji hayo wanayoyaelezea kama mabaya zaidi kutokea katika miezi ya hivi karibuni.

Aidha, Umoja wa Mataifa umefuta idadi ya waliojeruhiwa ya watu 110 iliyokuwa imetoa awali, na kusema kuwa idadi kamili ya walioathirika bado haijulikani.

Jeshi limekosolewa pakubwa kufuatia mauaji hayo lakini limelaumu ukosefu wa vifaa stahiki kuweza kukabiliana na kundi hilo. Pia limeshutumu wakaazi kwa kushirikiana na wanamgambo hao katika kuwapa taarifa.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.