Star Tv

Serikali imepokea msaada wa Faranga za Uswisi Milioni 15.75 sawa na shilingi Bilioni 39.59 kwa ajili ya kugharamia mradi wa uboreshaji na uimarishaji wa mfumo wa afya pamoja na kugharamia program ya kutokomeza Malaria nchini.

Msaada huo umepokelewa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bwana Doto James ambaye amesema lengo kuu la msaada huo ni uanzishwaji wa huduma ya msaada wa kitaalamu kwa Serikali chini ya utaratibu wa kituo cha kuimarisha mifumo ya afya kilichopo Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Bwana James alisema msaada huo utatumika kuwezesha mpango wa kudhibiti Malaria Tanzania ili kuondoa kabisa vifo vinavyotokana na malaria na kupanua wigo wa maeneo yasiyokuwa na malaria.

Bw. James alilifafanua  kuwa, hii ni mara ya pili katika kipindi cha siku 30 zilizopita kwa Serikali ya Uswisi kuipatia Tanzania msaada wa kuboresha masuala ya afya ambapo tarehe 6 Oktoba, 2020 nchi hiyo iliipatia Tanzania shilingi Bilioni 44.10.

Kwa upande wake Balozi wa Uswisi nchini, Mhe. Didier Chassot amesema tangu mwaka 2001, Uswisi kwa kushirikiana na Tanzania imekuwa ikitekeleza mapambano dhidi ya malaria kupitia program mbalimbali zenye lengo la kuisaidia nchi kufikia malengo iliyojiwekea kupitia Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano.

Aidha, Katibu Mkuu Wizara ya afya, Jinsia, Wazee na Watoto, Mkurugenzi wa Kinga Wizara hiyo, Dkt. Leonard Subi, alisema msaada huo utasaidia kuendeleza mafanikio yaliyopatikana hasa upatikanaji wa dawa na kuimarisha mifumo ya takwimu katika sekta ya afya nchini.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.