Star Tv

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli ametekeleza ahadi ya kulipa fidia ya zaidi ya shilingi bilioni 3 kwa wakazi ambao wanapisha ujenzi wa daraja la Kigongo Busisi jijini Mwanza.

Add a comment

Polisi mkoa wa Mwanza kwa kushirikiana na vyombo vingine vya kiusalama wamewakamata watu saba waliojifanya ni maofisa wa usalama.

Add a comment

Katibu mkuu wizara ya Maji Profesa Kitila Mkumbo ameagiza kuvunjwa kwa mkataba wa Mradi wa Maji wa Mbingu Vigaeni wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro unaogharimu zaidi ya shilingi Bilion 1.5 uliotakiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka 2019 lakini mpaka sasa umefikia asilimia 15 pekee .

Add a comment

Waziri wa elimu, sayansi na teknolojia Profesa Joyce Ndalichako ameamuru Mhandisi mshauri anayesimamia  mradi wa ujenzi wa chuo cha elimu na mafunzo ya ufundi stadi VETA mkoa wa Rukwa pamoja na mkandarasi wakamatwe na kuwekwa ndani kwa muda usiojulikana kutokana na kushindwa kukamilisha ujenzi wa chuo hicho kwa wakati  licha ya kuongezewa muda.

Taarifa yake;Brown Lawi Mtawa.

Add a comment

Baadhi ya wafugaji katika mikoa ya Pwani na Morogoro wameiomba serikali kufanya utafiti kubaini Dawa halisi ya kutokomeza wadudu wasumbufu wakiwemo Kupe weupe, wakisema pamoja na wengi wao kujitokeza kuogesha mifugo yao katika majosho yaliyopo lakini bado dawa zilizopo haziwasaidii .

Add a comment

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inafanya juhudi kuendeleza miradi ya maji safi na salama ambayo itawezesha changamoto ya upatikanaji wa huduma hiyo kuwa historia.

Add a comment

Kijana Devenja Kibotuo (35) mkazi wa Kijiji cha Uchau kusini Wilaya ya Moshi,mkoani Kilimanjaro  anadaiwa kufukua kaburi la mtoto wa dada yake aliyezikwa miaka 16 iliyopita kisha  kuotesha mgomba kwenye kaburi hilo. 

Add a comment

Vifaa vilivyokuwa  vikitumiwa na mamlaka ya vitambulisho vya taifa NIDA katika kuandikisha  vitambulisho vya taifa  kwenye  halmshauri ya wilaya ya Arusha iliyopo mkoani  Arusha ,vimeibiwa na watu wasiojulikana.

Mkuu wa wilaya ya Arumeru  Jerry Muro ametoa siku tatu kwa watu waliohusika  na wizi huo kuvirejesha vifaa hivyo kwa hiyari mara moja  kabla ya msako msako mkali kupitia vyombo vya dola kuanza.

Muro ametoa kauli hio katika ofisi hizo za halmashauri ya Arusha ambapo  amesema baada ya siku tatu  kupita watu walioiba vifaa hivyo wasiporejesha  hatua kali itatolewa kwa yeyote atakae kutwa na kifaa chochote ambacho ni mali ya serikali.

“Namimi niseme siko tayari kuona wilaya inahujumiwa, vitu vilivyoko kwenye wilaya vinahujumiwa alafu nikakaa kimya, niwaombe wananchi mtupatie ushirikiano lakini kwa wale waliohusika tunatoa siku tatu za kujisalimisha endapo vifaa havitarudishwa kwa hiyari tutachukua hatua.”-Jerry Muro-Mkuu wa wilaya ya Arumeru.

Muro amesema vifaa vilivyoibwa ni kamera mbili, stendi mbili, kompyuta mpakato mbili, kompyuta moja aina ya Desktop, stendi mbili, Extension mbili, pamoja na keyboad.

Amewaomba wananchi kutoa taarifa pindi watakapoona mtu yeyote anauza vifaa  hivyo vilivyoibiwa na kuwataka wasinunue kamera ,kompyuta ama vitu vilivyoibwa na kuwataka  wananchi hao kutoa taarifa pindi watakapona mtu yeyote anauza vifaa hivyo .

Aidha,mesema kuibiwa kwa vifaa hivyo si mara ya kwanza kutokea kwenye ofisi za NIDA za Arumeru na  upelelezi wakubaini juu ya wizi wa vifaa hivyo unaendelea.

Baadhi ya wafanyakazi katika ofisi hiyo  wameeleza hali waliyokumbana nayo baada ya kufika ofisini  na kulazimika kutoa taarifa kwa mamlaka husika.

Wilson Boaz ambaye ni mfanyakazi wa halmashauri ya wilaya ya Arumeru amesema alibaini wizi wa vifaa hivyo mara tu alipofika ofisini hapo.

nilipofungua nilikuta mlango uko wazi ndipo nilitoa taarifa kwa mlinzi aliyekuwa zamu”-Wilson Boaz, Mfanyakazi wa halmashauri wilaya ya Arumeru.

Kamanda wa polisi  mkoa Arusha Jonathan Shana amethibitisha kuripotiwa tukio hilo na amesema upelelezi umeshaanza na pindi utakapokamilika  taarifa rasmi ya polisi itatolewa.

 

                                                                                                                       Mwisho.

 

Add a comment

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza ACP Muliro Jumanne amekanusha taarifa zilizokuwa zinasambaa katika mitandao ya kijamii zikieleza kuwa kuna wanachama hao wa CHADEMA wametekwa jijini Mwanza.

Add a comment

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.