Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli ametekeleza ahadi ya kulipa fidia ya zaidi ya shilingi bilioni 3 kwa wakazi ambao wanapisha ujenzi wa daraja la Kigongo Busisi jijini Mwanza.
Add a commentRead more: DARAJA LA KIGONGO BUSISI MWANZA: Rais atoa zaidi ya Sh. Bil. 3 kulipa watakaopisha ujenzi
Polisi mkoa wa Mwanza kwa kushirikiana na vyombo vingine vya kiusalama wamewakamata watu saba waliojifanya ni maofisa wa usalama.
Add a commentRead more: WALIOJIFANYA MAOFISA USALAMA JIJINI MWANZA:Saba watiwa mbaroni.
Katibu mkuu wizara ya Maji Profesa Kitila Mkumbo ameagiza kuvunjwa kwa mkataba wa Mradi wa Maji wa Mbingu Vigaeni wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro unaogharimu zaidi ya shilingi Bilion 1.5 uliotakiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka 2019 lakini mpaka sasa umefikia asilimia 15 pekee .
Add a commentRead more: MRADI WA MAJI WA MBINGU VIGAENI KILOMBERO:Prof. Mkumbo aagiza mkataba kuvunjwa.
Waziri wa elimu, sayansi na teknolojia Profesa Joyce Ndalichako ameamuru Mhandisi mshauri anayesimamia mradi wa ujenzi wa chuo cha elimu na mafunzo ya ufundi stadi VETA mkoa wa Rukwa pamoja na mkandarasi wakamatwe na kuwekwa ndani kwa muda usiojulikana kutokana na kushindwa kukamilisha ujenzi wa chuo hicho kwa wakati licha ya kuongezewa muda.
Taarifa yake;Brown Lawi Mtawa.
Add a commentRead more: KUSHINDWA KUKAMILISHA UJENZI VETA:Mhandisi na Mkandarasi watiwa mbaroni Rukwa
Baadhi ya wafugaji katika mikoa ya Pwani na Morogoro wameiomba serikali kufanya utafiti kubaini Dawa halisi ya kutokomeza wadudu wasumbufu wakiwemo Kupe weupe, wakisema pamoja na wengi wao kujitokeza kuogesha mifugo yao katika majosho yaliyopo lakini bado dawa zilizopo haziwasaidii .
Add a commentRead more: WADUDU WASUMBUFU KWA MIFUGO-Kupe weupe washika hatamu.
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inafanya juhudi kuendeleza miradi ya maji safi na salama ambayo itawezesha changamoto ya upatikanaji wa huduma hiyo kuwa historia.
Add a commentRead more: MIRADI YA MAJI SAFI NA SALAMA: Serikali ya Zanzibar yafanya juhudi kuiendeleza.
Kijana Devenja Kibotuo (35) mkazi wa Kijiji cha Uchau kusini Wilaya ya Moshi,mkoani Kilimanjaro anadaiwa kufukua kaburi la mtoto wa dada yake aliyezikwa miaka 16 iliyopita kisha kuotesha mgomba kwenye kaburi hilo.
Add a commentRead more: MAAJABU YA DUNIANI:Kijana afukua kaburi na kupanda mgomba
Vifaa vilivyokuwa vikitumiwa na mamlaka ya vitambulisho vya taifa NIDA katika kuandikisha vitambulisho vya taifa kwenye halmshauri ya wilaya ya Arusha iliyopo mkoani Arusha ,vimeibiwa na watu wasiojulikana.
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro ametoa siku tatu kwa watu waliohusika na wizi huo kuvirejesha vifaa hivyo kwa hiyari mara moja kabla ya msako msako mkali kupitia vyombo vya dola kuanza.
Muro ametoa kauli hio katika ofisi hizo za halmashauri ya Arusha ambapo amesema baada ya siku tatu kupita watu walioiba vifaa hivyo wasiporejesha hatua kali itatolewa kwa yeyote atakae kutwa na kifaa chochote ambacho ni mali ya serikali.
“Namimi niseme siko tayari kuona wilaya inahujumiwa, vitu vilivyoko kwenye wilaya vinahujumiwa alafu nikakaa kimya, niwaombe wananchi mtupatie ushirikiano lakini kwa wale waliohusika tunatoa siku tatu za kujisalimisha endapo vifaa havitarudishwa kwa hiyari tutachukua hatua.”-Jerry Muro-Mkuu wa wilaya ya Arumeru.
Muro amesema vifaa vilivyoibwa ni kamera mbili, stendi mbili, kompyuta mpakato mbili, kompyuta moja aina ya Desktop, stendi mbili, Extension mbili, pamoja na keyboad.
Amewaomba wananchi kutoa taarifa pindi watakapoona mtu yeyote anauza vifaa hivyo vilivyoibiwa na kuwataka wasinunue kamera ,kompyuta ama vitu vilivyoibwa na kuwataka wananchi hao kutoa taarifa pindi watakapona mtu yeyote anauza vifaa hivyo .
Aidha,mesema kuibiwa kwa vifaa hivyo si mara ya kwanza kutokea kwenye ofisi za NIDA za Arumeru na upelelezi wakubaini juu ya wizi wa vifaa hivyo unaendelea.
Baadhi ya wafanyakazi katika ofisi hiyo wameeleza hali waliyokumbana nayo baada ya kufika ofisini na kulazimika kutoa taarifa kwa mamlaka husika.
Wilson Boaz ambaye ni mfanyakazi wa halmashauri ya wilaya ya Arumeru amesema alibaini wizi wa vifaa hivyo mara tu alipofika ofisini hapo.
“nilipofungua nilikuta mlango uko wazi ndipo nilitoa taarifa kwa mlinzi aliyekuwa zamu”-Wilson Boaz, Mfanyakazi wa halmashauri wilaya ya Arumeru.
Kamanda wa polisi mkoa Arusha Jonathan Shana amethibitisha kuripotiwa tukio hilo na amesema upelelezi umeshaanza na pindi utakapokamilika taarifa rasmi ya polisi itatolewa.
Mwisho.
Add a comment
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza ACP Muliro Jumanne amekanusha taarifa zilizokuwa zinasambaa katika mitandao ya kijamii zikieleza kuwa kuna wanachama hao wa CHADEMA wametekwa jijini Mwanza.
Add a commentRead more: Kukamatwa kwa wanachama wa CHADEMA:ACP Muliro akanusha taarifa hiyo.
Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]
Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]
Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]
Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.