Rais wa Tanzania, Samia Suluhu ametoa sababu ya kwanini taasisi za dini zinazotoa huduma katika sekta za afya na elimu zinatozwa na serikali, Ambapo amesema kuwa ni kwasababu baadhi zinafanya biashara na si kutoa huduma kama ilivyozoeleka.
Add a commentRead more: RAIS ATOA SABABU YA TAASISI ZA DINI KUTOZWA KODI.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Katibu Mkuu Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila kuhakikisha kuwa hadi kufikia tarehe 10 mwezi huu awe amefanya marekebisho ya kanuni za sheria ili wanunuzi wote wa madini ya Tanzanite wafanye biashara hiyo eneo la Mirerani.
Add a commentMkuu wa mkoa wa Mwanza Robert Gabriel ameyataka mashirika yasiyo ya kiserikali ambayo yanahusika na midahalo ya vijana kuhusu masuala ya amani nchini Tanzania na katika nchi za maziwa makuu kuzingatia sheria zinazoratibu usajili wa mashirika hayo.
Add a commentRead more: MRADI WA MTANDAO WA AMANI, UTULIVU MAZIWA MAKUU WAFUNGULIWA TANZANIA.
Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania, (TANAPA), limefungua fursa kwa wawekezaji wa ndani ya Tanzania kutembelea vivutio vinavyopatikana katika hifadhi za kanda ya Magharibi kkwa lengo la kuwekeza katika huduma mbalimbali. Hii inatokana na idadi ndogo ya watalii wa ndani na nje wanaotembelea hifadhi za ukanda huo.
Add a commentRais Samia Suluhu Hassan amesema serikali itaendelea kufanya kazi kwa kushirikiana na vyombo vya habari, ambapo amevitaka vyombo hivyo kuendelea kufuata kanuni na taratibu zilizowekwa.
Add a commentRead more: RAIS SAMIA AVIAHIDI VYOMBO VYA HABARI USHIRIKIANO.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imedhamiria kuendeleza zao la zabibu ili kuhakikisha linaleta tija kwa wakulima.
Add a commentMahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya imemuachia huru Mdude Nyagali baada ya kutomkuta na hatia katika kesi iliyokuwa ikimkabili ya kusafirisha madawa ya kulevya.
Add a commentWaziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali inathamini mchango wa Sekta Binafsi na Taasisi za Dini likiwemo kanisa Katoliki katika kuimarisha upatikanaji wa huduma mbalimbali za kijamii nchini.
Add a commentRais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema wakati umefika wa Wazanzibari kuungana pamoja katika vita dhidi ya usafirishaji na matumizi ya Dawa za kulevya pamoja na kuvitaka vyombo vya Ulinzi na Usalama kufanyakazi kwa weledi na ufanisi.
Add a commentRead more: RAIS MWINYI AAZIMIA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA.
Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]
Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]
Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]
Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.