Star Tv

Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa kipimo cha 5.9 Jumatano usiku limetikisa baadhi ya maeneo ya Tanzania hususani ukanda wa pwani na kishindo chake Kufika mpaka katika baadhi ya maeneo ya nchi jirani ya Kenya.

Kwa mujibu wa taasisi ya uchunguzi wa jiolojia ya Marekani, 'US Geological Survey (USGS)', kitovu cha tetemeko hilo ilikuwa katika eneo lililopo kilomita 66 mashariki mwa mji mdogo wa Vikindu, Mkoani Pwani.

Tetemeko hilo lilipiga katika kina cha kilomita 15.5 (maili 9.6), lililotokea jijini Dar Es Salaam eneo linalojulikana kama jiji kuu la biashara nchini.

Mpaka sasa hakuna uharibifu wowote ulioripotiwa baada ya tetemeko hilo.

Tetemeko hilo imekuja siku chache baada ya wakazi wanaoishi pembezoni mwa ziwa Baringo nchini Kenya kuripotiwa kuwa na tetemeko baada ya kiwango cha maji kujaa kwa sababu ya mvua zinazoendelea.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.