Mgombea Urais kwa tiketi ya chama cha ACT-Wazalendo Bernard Membe tayari amechukua fomu ya kuwania Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Agosti 07, 2020 katika Makao Makuu ya Tume ya Uchaguzi (NEC) Dodoma.
Membe aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania katika utawala uliopita. wa awamu ya nne ambao ulikuwa chini ya Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete aliongozana na mgombea mwenza Profesa Omar Fakih Hamad.
Membe pamoja Prof. Omar wamesindikizwa na viongozi wa chama hicho, akiwemo Mwenyekiti wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad na Katibu Mkuu wake, Ado Shaibu.