Star Tv

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) amewasili nchini Madagascar kuchukua dawa ya Corona.

Baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege nchini humo Waziri Kabudi alipokelewa na mwenyeji wake ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Madagascar Mhe. Tehindrazanarivelo Djacoba.

Akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Madagascar Mhe. Tehindrazanarivelo Djacoba As Oliva mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Antananarivo Waziri Kabudi alionekana katika picha nyingine  anakabidhiwa maboksi ya dawa hizo.

Kufikia sasa watu 509 kutoka 480 ndio walioambukizwa ugonjwa wa corona  hapa nchini mara baada ya Wizara ya Afya ya Zanzibar hapo jana kutangaza wagonjwa wapya 29.

Mnamo Mei 3, Rais wa John Pombe Magufuli alisema kuwa atatuma ndege kwenda Madagascar kufuata dawa hiyo ya mitishamba, Japokuwa Shirika la Afya Duniani limesema ni muhimu dawa zinazosemekana kuwa na uwezo wa kutibu virusi vya corona kufanyiwa majaribio kwanza kabla ya kuanza kutumiwa.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.