Star Tv

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa amesema mazishi ya aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Mtwara Evodi Mmanda yatafanyika Mtwara na kuhudhuriwa na watu wasiozidi kumi tu.

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara amesema lengo la watu kumi kuhudhuria mazishi ya Bwana Mmanda ni kuendelea kusimamia msimamo wa Wizara ya Afya juu ya kuzuia mikusanyiko katika kipindi hiki cha maambukizi ya Corona.

Mazishi ya Mkuu wa Wilaya huyo yatasimamiwa na serikali na tayari familia ya marehemu imeridhia mwili wa mwanafamilia wao kuzikwa mkoani Mtwara.

Mkuu wa Mkoa amesema Bwana mmandi alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya Moyo na Sukari ambapo hali yake ilibadilika siku ya Ijumaa na kulazwa katika hospitali ya Ligula.

Marehemu Evod Mmand, amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo, ambapo alianza kuhudumu katika nafasi ya ukuu wa Wilaya mwaka 2016, baada ya kuteuliwa na Rais John Pombe magufuli.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.