Star Tv

Wafanyabiashara wametakiwa kuendesha biashara zao kwa uadilifu na huruma na kamwe wasitumie uwepo wa janga la Covid-19 kuwawekea mazingira magumu wananchi kwa kuwauzia bidhaa kwa bei kubwa hasa kipindi cha mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein ameyasema hayo leo katika risala ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani aliyoitoa kupitia vyombo vya habari, ikiwa ni utaratibu wake aliuoweka unapokaribia mwezi huo Mtukufu kila mwaka.

Alhaj Dk. Shein amewaeleza wananchi kuwa mwaka huu wa 2020 mwezi Mtukufu wa Ramadhani unakaribishwa huku kukiwa na mtihani wa maradhi yanayosababishwa na virusi vya Korona vinavyojulikana kwa jina la COVID 19.

Rais Dk. Shein amewagiza Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na Masheha wahakikishe kwamba katika maeneo yao ya utawala wanavidhibiti vitendo vyote vinavyoweza kuathiri juhudi na mipango ya Serikali katika kupambana na maradhi hayo ikiwemo mikusanyiko ya watu.

Aidha, Alhaj Dk. Shein aliwanasihi wananchi wote wasisikilize taarifa zisizo rasmi wanazozitoa watu wasiohusika ambao hawana mamlaka ya Kiserikali ya kutangaza taarifa za Serikali.

Rais Shein amewatakia wananchi wote kheri na Baraka za Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.