Star Tv

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeidhinisha azimio la kusitisha mapigano kwa mara ya kwanza tangu kuzuka kwa mgogoro nchini Libya, na kuzitaka pande zote husika kufikia makubaliano ya kudumu.

Mwezi Januari mwaka huu pande zinazokinzana nchini Libya zilifikia mkataba wa kusitisha mapigano, lakini mkataba huo mpaka sasa bado unalegalega kutokana na kuwa mapigano yamekuwa yakiendelea na kila upande ukishutumu upande mwingine kukiuka mkataba huo.

Azimio hilo limepitishwa baada ya mazungumzo yaliyodumu zaidi ya wiki tatu, huku kukionekana mgawanyiko wa kimataifa unaoendelea licha ya kuonyesha umoja wao katika mkutano uliofanyika kwenye mji mkuu wa Ujerumani, Berlin, Januari 19 mwaka huu.

Mkutano huo ambao rais wa Urusi na Uturuki walishiriki kila mmoja alikuwa akionyesha kuunga mkono kambi moja hasimu iliyopo  nchini Libya.

Azimio hilo ambalo bado halijafikiwa  linataka kuwepo kwa makubaliano ya kudumu ya kusitisha mapigano nchini Libya, kabla ya yote na bila masharti.

Urusi inashutumiwa kwa miezi kadhaa kuunga mkono usafirishaji wa maelfu ya mamluki wa kundi la Wagner, linalodaiwa kuwa na uhusiano wa karibu na ikulu ya rais wa Urusi, kwenda nchini Libya kumsaidia Khalifa Haftar ambaye amekuwa akitafuta kuudhibiti mji wa Tripoli  tangu Aprili 4, 2019.

                                                                         Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.