Star Tv

Gavana wa Benki kuu Tanzania Florens Luoga amesema muda sio mrefu itaweka kanuni za kuhakikisha fedha zinazotokana na madini zinarudi Nchini kwani wawekezaji walikua wnadanganya kwa sababu ya kuwa na akaunti za benki nje ya nchi na kusababisha fedha kutorudi Nchini.

Taarifa na Salma Mrisho.

Akiwa Mkoani Geita kwa ziara ya siku moja na kutembelea mgodi wa dhahabu wa geita pamoja na maeneo mengine kuangalia hali ya uzalishaji wa dhahabu unavyofanyika.

Luoga  amesema kuwa haiwezekani Tanzania kuwa na dhahabu za kutosha halafu hakuna eneo la kuhifadhi dhahabu na kuongeza kuwa hivi karibuni kutakua na kanuni za uhifadhi wa dhahabu.

Uwepo wa masoko ya dhahabu umechangia kupatikana kwa mapato ambapo kuanzia machi 2019 hadi januari 2020 umeshazalisha tani tatu za Dhahabu zenye thamani ya bilioni 362.

Suala la kituo cha kuhifadhi dhahabu nalo limezungumzwa na kuonekana kama changamoto inayowakabili wawekezaji hao ambapo BOT wamesema  watakaa na kulifanyia kazi.

Halmashauri ya Mji wa Geita tayari imetenga maeneo ya kimkakati kwa shughuli mbalimbali za sekta ya madini.

                                                           Mwisho.

 

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.