Basi la kampuni ya Premier linalofanya safari zake kati ya Mwanza na Mbeya limegongana uso kwa na lori lenye namba za usajili T486 ANU ambalo lilikuwa likivuta tela lenye namba T 775 APT na kusababisha vifo vya Watu wawili na majeruhi nane.
Ajali hiyo ambayo imehusisha basi na lori imetokea majira ya asubuhi katika kijiji cha Inyala wilaya ya Mbeya mkoani Mbeya.
Jitihada zilofanywa ni kuliondoa lori ambalo lilikuwa limeegeshwa barabarani ili kuruhusu magari mengine yaweze kupita na kuendelea na safari kwenye barabara hiyo pamoja na kuwakimbiza majeruhi hospitali.
Mwisho.