Star Tv

Serikali imemtahadharisha mkandarasi anayetekeleza mradi mkubwa wa ujenzi wa kituo cha Daladala Manispaa ya Morogoro kuwa huenda akabomoa na kuanza kujenga upya kwa gharama zake jengo la Utawala linalogharimu kiasi cha shilingi Milioni 400 itakapobainika kujengwa chini ya kiwango.

Habari na  Omary Hussein

Kituo hicho cha Dalalada manispaa ya Morogoro ambachoo utekelezaji wake unagharimu zaidi ya shilingi Bilion 5 ambazo ni fedha za mkopo kutoka benki ya dunia, ukitekelezwa na mkandarasi mzalendo kampuni ya Nandra Engenearing Constractin LTD, ya Jijini Dar es salaam.

Waziri wa nchi ofisi ya Rais Selemani Jafo ambaye amefika kukagua mradi huo wa ujenzi wa kituo cha daladala amesema kuwa wasiwasi wake ni muonekano wa jengo la Utawala ambalo amemsihi mkandarasi kuhakikisha jengo hilo linajengwa vyema na mkandarasi huyo ameaswa kuzingatia makubaliano ya mkataba.  

Katika hatua nyingine akiwa mkoani hapa waziri Jafo amekagua na kuzindua shule mpya ya Mfano kwa shule za Sekondari za serikali nchini, shule ya Sekondari Mji mpya iliyogharimu kiasi cha shilingi Bilion 1.4.

Awali  baadhi ya viongozi mkoa huo wamesema kupatikana kwa shule hiyo ya Mfano, kutaongeza ushindani katika mitihani ya kitaifa wakitamani shule hiyo kupanda hadhi kuchukua pia wanafunzi wa kidato cha tano na sita.

Shule hiyo ya sekondari ambayo utekelezaji wake umegharimu kiasi cha bilioni 1 na million 400 fedha ambazo ni matunda ya Mradi wa Reli ya kisasa, inatajwa kuwa ndio shule ya mfano kwa shule zote za serikali nchini hususani ngazi ya kata, na utekelezaji wake umezingatia miundombinu ya wenye mahitaji maalum, maktaba ya kisasa na maabara kwa masomo yote ya sayansi.

                                                                                     Mwisho.

 

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.