Star Tv

Aliyewahi kuwa  katibu  wa baba wa Taifa hayati mwalimu Julius Kambarage Nyerere, mzee Samuel Kasori amesikitishwa na hatua ya serikali ya kukitelekeza chuo cha utafiti wa kilimo na  mifugo Uyole jijini Mbeya, ambacho kilianzishwa na mwalimu Nyerere kwa misingi maalumu ya kukuza na kuendeleza sekta ya kilimo nchini.

Mzee Kasori amesema kuwa kwa mara ya kwanza alifika chuoni hapo akiwa na mwalimu Nyerere mika ya 1990.

Matarajio yake ilikuwa ni kutaka kuona miundombinu ya  chuo hicho cha kilimo Uyole kikiendelea kung’aa na kufanya kazi zilizo kusudiwa na baba wa taifa.

Lakini uchakavu wa majengo na miundombunu mibovu ya barabara ndani ya chuo hicho ilimuhuzunisha katibu Kasori ambaye ni mwalimu Nyerere.

“Akili zetu katika karne ya 21 unaaamua kudhoofisha usafiri wa reli, bandari, pamoja na vituo vya utafiti n ahata elimu kwa ujumla”; Samuel Kasori aliyewahi kuwa katibu wa Mwl. Nyerere.

Baada ya kukutana na watumishi wa chuo hicho aliweza kuwaeleza kwamba  dhamira ya baba wa taifa kuweka alama ya taasisi hiyo kwa kukianzisha ilikuwa ni kuweza kujitegemea katika chakula na ndio maana chuo hicho kilianzishwa.

Ukosefu wa bajeti ya kutosha kwa ajili ya kuendeleza taasisi hiyo umetajwa kuwa miongoni mwa kikwazo kinachowakwamisha watafiti kutafiti na kukuza teknolojia ya mifugo hapa nchini.

Chuo cha utafiti wa kilimo na mifugo Uyole ni moja ya taasisi za serikali zilizoashwa maalumu kwa ajili ya kutafiti na kukuza technologia ya kilimo na mifugo hapa nchini.

Mwisho.

 

 

 

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.