Star Tv

Naibu wa  Waziri wa Ardhi Nyumba na  maendeleo ya Makazi  Angelina Mabula amesema wakulima  wanapaswa kupimiwa maeneo yao ili kutokemeza migogoro ya ardhi nchini kwakuwa wataweza kujipatia hati miliki  ya ardhi zao.

 Naibu waziri  huyo amebainisha hayo  wakati akikabidhi hati miliki za kimila mia moja kwa  wakulima wadogowadogo  katika kijiji cha Litowa  Mkoani Ruvuma ambazo zimetolewa na mtandao wa wakulima Mviwata kwa kushirikiana na Halmsahuri ya Wilaya ya Songea.

 Mabula amesema hati hizo za kimila zilizotolewa zimelenga kutokemeza migogoro ya ardhi pamoja na kuongeza uzalishaji wenye tija

Kwa upande wake Mratibu wa MVIWATA Mkoa wa Ruvuma Laika Haji amesema utoaji wa hati hizo miliki umelenga kulinda usalama wa  ardhi huku Mwenyekiti wa kijiji hicho  Fabiani Shawa akiamini utolewaji wa hati hizo miliki utasaidia kukuza kilimo na kupunguza migogoro ya ardhi ambayo inapoteza muda wa wakulima kuisulisha.

Zaidi ya hati za Kimila 1700 zimetolewa katika Mkoa wa Ruvuma katika wilaya za tunduru, Madaba na Songea Vijijini ambapo  zaidi ya wananchi 1700 tayari wananufaika na urasimishaji huo wa ardhi.

 

                                                                                         Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.