Star Tv

Wakazi wa Kijiji cha Tatwe wilayani Rorya mkoani Mara wamekumbwa na maporomoko  ya ardhi ambayo yamesababishwa na  mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.

Mvua hizo zimeelezwa kusababisha  hasara kubwa kwani idadi kubwa ya ekari za mashamba na baadhi ya mifugo pamoja na kuathiri kaya kumi zinazohitaji msaada wa hali na mali.

Kutokana na mvua hizo kuleta athari kubwa katika kijiji hicho kaya kumi ambazo zimeathirika zinaomba kupatiwa misaada mbalimbali ikiwemo vyakula pamoja na kuhamishiwa kwenye eneo salama ili kuepuka maafa.

 Mwenyekiti wa Kitongoji cha Sang'ombe kijiji cha Tatwe Wilayani Royra Mkoani Mara Kevin Chacha  amesema.“Naomba serikali isaidie hawa wakazi wa Kijiji changu kwa mbinu zozote  ambazo wataweza kuwasaidia, kama ni chakula wapewe”

Lameck Airo ambaye  ni mbunge wa jimbo la Rorya  akiongozana na  mwenyekiti wa CCM wa Wilaya hiyo  Charles Ochele wamefika katika kitongoji cha Sang'ombe kilichoko katika  kijiji cha Tatwe ili kujionea hali halisi ya tukio hilo  ambalo halijawahi kutokea na kuwapa pole wakazi waliofikwa na janga hilo.

“Mimi toka nimezaliwa sijawahikuona tukio la jabu Tanzania nzima kama nililoliona leo kama chanzo ni maji yameweza kulipuka na baada ya kulipuka ikasababisha mto mkubwa kama huu ni maajabu na  nitawachangia wananchi milioni moja”

Maporomoko hayo ambayo ni ya kwanza kutokea katika kijiji cha Tatwe Wilayani Rorya na yametengeneza  korongo lenye urefu wa zaidi ya kilometa mbili  na kuacha Historia kwa wakazi wa Kijiji hicho cha Tatwe.

                                                                                         Mwisho

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.