Star Tv

Kamati ya ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mara imeviagiza vyombo vya dola kuwasaka vijana watatu waliokimbilia nchi jirani ya Kenya baada ya kumchoma mkuki shingoni na kumuua mwalimu Justin Sospeter Ogo wa shule ya sekondari Itiryo.

 Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa mkoa wa Mara Adam Malima akizungumza na vyombo vya hanari ofisini kwake kufuatia kuelezwa juu ya taharuki toka kwa walimu kuhofia usalama wao kutokana na vijana hao kumuua mwalimu mwenzao wakati alipokuwa akiwasindikiza wenzake kwenda kusimamia mitihani.

 Akizungumzia hali hiyo mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Mara Adam Malima amewataka walimu kuendelea na majukumu yao bila hofu.

 Pamoja na suala hilo Malima amepiga marufuku shughuli zote za tohara mpaka hapo vijana hao watatu watakapopatikana.

Hivi karibuni vijana wanane waliokuwa wakijiandaa kufanyiwa tohara walimpiga mkuki wa shingo Mwalimu Justin Ogo wa shule ya sekondari Ogoo huku wakidaiwa kumvunja mkono mwanafunzi wa kidato cha nne kwa madai ya kuonyesha ujana wao kabla ya tohala.

 

                                                                                   Mwisho

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.