Star Tv

Umoja wa Makanisa Jijini Mwanza umeunga mkono Hatua ya serikali ya kupiga marufuku ibada  zinazoendeshwa na Diana Bundala anayejiita Mfalme Zumaridi baada ya kubainika ibada hizo zinafanyika kinyume na sheria na taratibu za nchi.

 

Ikiwa bado ni hali ya kushangaza kwa wengi waliosikia na kushuhudia Serikali ikilifungia Kanisa la Mfalme Zumalidi Jijini Mwanza ikidawa ibada na imani za kanisa hilo hazithibiti matakwa ya ukristo.

 Umoja wa makanisa Jijini Hapa unaoundwa na mabaraza ya TEC, CCT na CPCT umevunja ukimya na kutoa tamko rasmi kuiunga Mkono serikali juu ya hatua iliyochukua dhidi ya kanisa hilo.

 Kanisa hilo linadaiwa kutumia usajili wa Kanisa la pentekoste ambapo umoja huu umesema hali hiyo inakwenda kuchafua wakikristo neno kwa wizara ya mambo ya ndani yakwamba hali hiyo ikitokea inachafua wakristo wote.

 Askofu. Philipo Mafuja ambaye ni mwenyekiti wa umoja wa makanisa jijini Mwanza amesema  “Kama mtu amefika mahala anasema kikristo amepitwa na wakati ni lazima ataumiza hisia za watu wengi”

 Pia Askofu Zenobius Isaya ambaye ni Katibu wa baraza la makanisa ya kipentekoste amesema “Kama mtu amefika mahala alikuwa anajiita Mungu sasa mtu akishajiita Mungu ni kejeli ya kiwango cha juu na ndio maana alikuwa na maneno mengi anasema Mwanza hii hakuna wachungaji kama mimi”

 Novemba 18 mwaka huu, kamati ya Ulinzi na Usalama Ikiongozwa na Mkuu wa wilaya ya Nyamagana walitembelea kanisa hilo na kutoridhishwa  na utaratibu wa uendeshwaji wa ibada na hivyo kufikia hatua ya kulifunga.

                                                                                                     Mwisho.

 

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.