Star Tv

Serikali imesitisha kwa muda usiojulikana shughuli za uchimbaji wa Madini ya Dhahabu katika machimbo ya Shilalo wilayani Misungwi mkoani Mwanza ili kupisha uchunguzi wa mgogoro uliojitokeza baina ya kikundi cha Mlimani ambao ni waanzilishi wa uchimbaji, mmiliki wa shamba na  mwekezaji mpya aliyejitokeza kuwekeza eneo hilo.


Ni baadhi ya wachimbaji wadogo  katika Machimbo ya Shilalo yaligunduliwa na wachimbaji hao Mwaka 2017 yakiwa na  yanajumla ya  madura ya uchimbaji 57 ambapo 38 yamesitishwa na serikali  kuendelea na uchimbaji huo.

Machimbo hayo yaliyositishwa tangu Oktoba Saba mwaka huu ,Chanzo cha mgogoro  ni  mmoja wa wamiliki wa shamba linalochimbwa kudaiwa  kuweka mwekezaji mwingine huku wanakikundi cha Mlimani group wakiwa hawafahamu hatima yao.

Mmiliki wa Shamba hilo Wilbert Magwatamula amesema shamba hilo amelinunua tangu mwaka 1982 na anamtambua kikundi cha Mlimani kuwa ndio wawekezaji wa mwanzo.

SB: Wilbert Magwatamula   Mmiliki wa Shamba

Meneja  Msaidizi wa kikundi cha Mlimani Dastan Henry ambao ndiyo walioanza kuchimba machimbo hayo amebainisha chanzo cha Mgogoro huo  na manufaa ambayo  yanapatikana kutokana na  machimbo hayo kwa wanakijiji.

SB: Dastan Henry - Meneja msaidizi wa kikundi cha Mlimani

Hata  hivyo uongozi wa kijiji  cha Shilalo bado unatia shaka na mwekezaji  mpya anayedaiwa.

SB: Kang'wa  Nzugamawe  Sahani - M/Kiti wa Kijiji cha Shilalo  
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella ametoa kauli ya serikali wakati mgogo huo ukitafutiwa ufumbuzi .  

SB: John Mongella - Mkuu wa Mkoa wa Mwanza

Machimbo ya Shilalo yanakadiriwa kuajiri wananchi elfu 6 wanaotegemea mgodi huo kuendesha maisha yao ya kila siku
Mwisho

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.