Star Tv

Wakazi wa mji wa Maswa mkoani Simiyu wameilalamikia Mamlaka ya Maji na Usafi wa mazingira, (MAUWASA), kwa kitendo cha kupiga marufuku wamiliki wa mabomba ya maji kutoa huduma ya maji kwa watu wasiokuwa na huduma hiyo.

Baadhi ya waananchi wasiokuwa na mabomba ya maji wameilalamikia maamlaka ya maji kuweka zuio la kupata huduma ya maji kwa ndugu na jamaa zao. Hali ambayo wamesema inawaweka katika wakati mgumu kupata huduma ya maji safi na salama kutokana na wao kutokuwa na uwezo wa kumiliki mabomba ya maji katika makazi yao. Mkurugenzi Mtendaji wa mamlaka ya maji na usafi wa mazingira mjini Maswa (MAUWASA), Anacleth Tibita amewataka watu wasiokuwa na uwezo wa kumiliki mabomba ya maji kupata huduma hiyo katika vituo vilivyopangwa. Kwa siku za hivi karibuni mamlaka ya maji mjini maswa imekuwa ikifanya msako wa kusitisha huduma ya maji kwa wateja wake wanaotoa maji kwa watu wasiokuwa na huduma hiyo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.