Star Tv

Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Mara imekamata kilo tano za mchanga wenye madini ya dhahabu ukiwa na thamani ya shilling milllioni ishirini na tano ukitoroshwa kwenda kutafutiwa soko maeneo mengine.

Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa Mara Adam Malima ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa akizungumza na viongozi na wachimbaji madini toka katika mgodi wa Ilasanilo Buhemba kufuatia kuwepo kwa taarifa juu ya wao kukataa kujenga ukuta kwa lengo la kuzuia utoroshaji madini. Serikali haipo tayari kuona watu wachache wanakwamisha shughuli hiyo na kukosa mapato hivyo kama hawapo tayari mgodi huo utafungwa. Viongozi wa wachimbaji wadogo katika mgodi huo wanakili kuwepo kwa tatizo hilo huku wakisema ujenzi wa ukuta utasaidia kukabiliana na wimbi la wizi wa madini. Ni mwezi mmoja sasa tokea kufunguliwa kwa mgodi wa Ilasanilo Buhemba baada ya kufungwa kwa muda mrefu kutokana na baadhi ya mashimo kudaiwa kuhatalisha maisha ya wachimbaji.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.