Star Tv

Shirika la ugavi wa umeme TANESCO Mkoani Kagera limewaonya wajasiriamali wanaotumia umeme kwa njia za wizi ili kuutumia katika mitambo yao ya kutega senene  hususani nyakati za usiku.

Oparesheni ya kushtukiza iliyofanywa na maafisa wa TANESCO katika kijiji cha Ngarama  kata ya Katoro wilayani Bukoba imebaini asilimia kubwa ya nyumba katika kijiji hicho kuunganishiwa umeme kwa njia za wizi pasi na kufuata utaratibu. Afisa Usalama wa TANESCO mkoani Kagera Stephen Maganga amesema umeme unaoibiwa ni ule unaotumika katika mitambo ya kutegea senene nyakati za usiku na kuwataka wananchi hao kuacha la sivyo hatua kali za kisheria zitachuliwa dhidi yao ikiwa ni pamoja na kuondoa nguzo zote za umeme katika kijiji hicho.

Pamoja na wakazi wengi wa kijiji hicho kukimbia mara baada ya kusikia uwepo wa oparesheni hiyo,Mwenyekiti wa serikali ya kijiji  Abdulkarim Twaha amelitaka shirika hilo kufanya oparesheni za mara kwa mara pamoja na kuchunguza baadhi ya watumishi wa shirika hilo wanaoshirikiana na vishoka kufanya hujuma hizo maafisa hao walilazimika kufanya kazi ya ziada ya kuwaweka chini ya ulinzi baadhi ya wakazi waliobainika kushiriki katika hujuma hizo.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.