Kamishna wa Operesheni na Mafunzo Liberatus Sabas ameongoza operesheni katika Wilaya ya Kibiti, Kijiji cha Rungungu eneo ambalo mauaji yalilindima na kutikisa Mkoa wa Kipolisi Rufiji katika Wilaya ya Ikwiriri,Mkuranga na Kibiti eneo ambalo lilikabiliwa na mauaji ya Viongozi wa Dini, Viongozi wa Kisiasa, Askari Polisi pamoja na watumishi wengine wa Serikali.
Mauaji hayo yaliendeshwa na kikundi cha kiarifu ambacho kiliamua kujichukulia eneo katika kijiji cha Rungungu walilotumia kama eneo la makazi na mazoezi kabla hawajaenda kutimiza azima yao ya uharifu.Katika hatua hiyo Kamishna CP Sabas amesema Jeshi la Polisi kwa
kushirikiana na Vyombo vingine ya Ulinzi na Usalama na kuweza kufanikiwa kulitokomeza kundi hilo la kihalifu ambalo lilikuwa limeweka himaya katika mapori hayo, ameongezea kwa kusema katika Operesheni iliyofanywa katika eneo hilo wamehakikisha pori hilo liko salama na hakuna kitu chochote walichoweza kukipata porini humo.