Star Tv

Kamishna wa Operesheni na Mafunzo Liberatus Sabas ameongoza operesheni katika Wilaya ya Kibiti, Kijiji cha Rungungu eneo ambalo mauaji yalilindima na kutikisa Mkoa wa Kipolisi Rufiji katika Wilaya ya Ikwiriri,Mkuranga na Kibiti eneo ambalo lilikabiliwa na mauaji ya Viongozi wa Dini, Viongozi wa Kisiasa, Askari Polisi pamoja na watumishi wengine wa Serikali.

Mauaji hayo yaliendeshwa na kikundi cha kiarifu ambacho kiliamua kujichukulia eneo katika kijiji cha Rungungu walilotumia kama eneo la makazi na mazoezi kabla hawajaenda kutimiza azima yao ya uharifu.Katika hatua hiyo Kamishna CP Sabas amesema Jeshi la Polisi kwa
kushirikiana na Vyombo vingine ya Ulinzi na Usalama na kuweza kufanikiwa kulitokomeza kundi hilo la kihalifu ambalo lilikuwa limeweka himaya katika mapori hayo, ameongezea kwa kusema katika Operesheni iliyofanywa katika eneo hilo wamehakikisha pori hilo liko salama na hakuna kitu chochote walichoweza kukipata porini humo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.