Star Tv

Wadau wa Uwindaji wa Kitalii wameishukuru serikali ya Marekani baada ya kuondoa zuio kwa kampuni zinazojihusisha na sekta hiyo vya kuuza Nyara za Wanyamapori hasa Simba baada ya kuthibitika kuwa sehemu ya mapato yatokanayo na uwindaji huo yanatumika vyema katika shughuli za Uhifadhi .

Serikali ya Marekani ilijiweka kando na Ununuzi wa Nyara kutoka Tanzania tangu mwaka 2014 huku Taifa hilo  likitajwa kuwa Mdau mkubwa wa Nyara hizo hasa Simba. Lakini kwa sasa milango ipo wazi ,baada ya serikali ya Marekani kuridhishwa na mwenendo wa Makampuni hayo na hii ikitokana na uwajibikaji uliofanywa na mamlaka ya usimamizi wa  wanyamapori katika kuendesha zoezi zima la Ulinzi wa Wanyamapori. Naibu Kamishna wa Utalii na Biashara kutoka Mamlaka ya Wanyamapori Nchini Iman Nkui amesema, kufunguliwa kwa soko hilo kunafatiwa na ujio wa wataalam kutoka nchini Marekani kuja kuona ni jinsi gani shughuli za uwindaji zinavyosaidia Uhifadhi na Jamii. Aidha Mkui ameongeza kuwa kwa sasa Mamlaka hiyo inasubiri taarifa rasmi ya kufunguliwa kwa soko hilo ambalo litaongeza Pato la Taifa kupitia Sekta hiyo.

 

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.