Star Tv

Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zuberi  amewahimiza Waislamu hasa wanaokaa katika mikoa yenye dhahabu kuondoka katika hali ya kawaida ya kuendeisha dini tupu bali iwe dini na uchumi kwa lengo la kuwa tegemezi lakini kuwa na uchumi imara utatoa fursa ya kujisimamia na kuendesha  miradi mbalimbali ya kimaendeleo.

Ni  ya Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zuberi amefanya  ziara ya siku mbili lengo ni kutembelea na kuona miradi na uwekezaji uliofanya na viongozi wa kiislam  katika mkoa wa Geita, na kubainisha  kuwa zama za sasa ni za kuleta maendeleo na sio migogoro ambayo inadidimiza juhudi za kuleta maendeleo. Baraza kuu la Waislamu  Tanzania makao makuu limeanzisha kitengo cha uchumi na maendeleona huku viongozi wakitakiwa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha fursa zilizopo mlangoni zinatumika huku Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel  akisema kuwa Viongozi wana wajibu wa kuibadilisha jamii hasa kwa kuwaongoza kwa maadili ambayo yanampendeza Mungu yenye kutoa haki pasi na ubaguzi. Mufti Zubeir amezindua msikiti Buseresere Wilayani Chato, Kiwanja cha ujenzi  shule ,eneo la uchimbaji wa dhahabu Wilayani Bukombe na Mradi wa Shule Geita Mjini.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.