Shehena ya samaki aina ya dagaa zinazokadiliwa kufikia tani elfu kumi na sita zenye thamani ya zaidi ya shiring million 38 zimekamatwa na vikosi vya udhibiti rasilimali za ziwa Victoria mkoani Mara zikiwa ndani za Boti mbili za Mv Ing’ang’a zikitoroshwa kwenda nchi jirani ya Kenya kuuzwa.
Ni shehena ya samaki aina ya dagaa yenye thamani zaidi ya shilling million 38 waliokuwa wakitaka kutoroshwa kwenda nchini Kenya kinyume cha sheria kwa kulipiwa ushuru kidogo imekamatwa na maafisa wa udhibiti rasilimali za ziwa Victoria mkoani Mara.
Akizungumzia tatizo hilo mkuu wa wilaya ya Musoma Dr Vicenty Naano amesema walibaini uwepo wa boti hizo mbili za Mv Ing’ang’a zikiwa zikiwa na mzigo huo zikitaka kuanza safari kwenda nchi jirani huku mmiliki wa boti hizo akishindwa kusema ukweli.
Nao baadhi ya wafanyabiashara katika mwalo wa Mwigobero wanadai kuwa mzigo huo wameuuza kwa wafanyabiashara toka nchi jirani ya Kenya.
Kwa mujibu wa mkuu wa vikosi vya uvuvi mkoani Mara,wafanyabiashara hao walililipia tani nne tuu huku wakikwepa kulipia tani zaidi ya elfu kumi na mbili za samaki hao.